Saturday, January 31, 2015

Godbless Lema Amshambulia Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja......Asema Anamhujumu IGP Mangu


MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), jana alimshambulia kwa maneno makali Kamishna wa Oparesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Paul Chagonja, kuwa anaweza kuwa anashirikiana na majambazi wanaovamia vituo vya polisi na kupora silaha.
 
Lema alitoa maneno hayo makali ya kumshambulia Chagonja bungeni jana, wakati akichangia taarifa za Kamati za Bunge za Hesabu za Serikali Kuu (PAC) na Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC).
 
Akichangia hoja hizo, Lema aliliambia Bunge kuwa Chagonja anaweza kuwa anahusika katika matukio ya ujambazi katika vituo vya polisi kwa sababu anataka kudhoofisha utendaji kazi wa Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Ernest Mangu.
 
Katika maelezo yake hayo, Lema alilifananisha taifa na chumba kinachotumiwa na vijana wa kihuni kuishi ambacho hakina utaratibu unaoeleweka wa muda wa maakuli na malazi.
 
“Mheshimiwa Mwenyekiti, geto ni mahali ambapo watu wanaishi bila kufuata utaratibu, yaani katika geto, wakati wa kulala anayewahi ndiye anayelala kitandani.
 
"Geto chakula kinapopikwa kinaweza kuliwa hata kama hakijaiva, kwa hiyo nchi hii naifananisha na geto kwa sababu watu wanaiba fedha za umma kama wanavyotaka.
 
“Katika ripoti za Bunge zilizosomwa hapa jana (juzi) zimejaa wizi, kila ukurasa wa taarifa ya Zitto ni wizi tu, wizi tu, hivi huu wizi utakwisha lini? Hata zile bunduki zinazoibwa katika vituo vya polisi zinaweza kuwa ni ‘sabotage’ (hujuma), zinazofanywa na Chagonja dhidi ya IGP,” alisema Lema.
 
Alisema amefanya uchunguzi wake binafsi uliobaini kuwa Jeshi la Polisi limegawanyika na kwamba haamini kama Rais Jakaya Kikwete amekwishafanya mabadiliko ya uongozi ndani ya jeshi hilo.

Sunday, January 18, 2015

VIDEO ZA SHOW YA NYAKABAYA



NYAKABAYA AU CHABHANYA ATISHA MNADANI SENGEREMA KWA SHOW BABUKUBWA ALIYO IPIGA HAPO JANA


 MSANII HUYU AMEKUWA MAARUFU SANA KWA JINA LA CHABHANYA NA KUJIKUTA ANAPATA UMARUFU SANA WILAYANI SENGEREMA HUSUSA NI MAENEO YA BUCHOSA.
NYAKABAYA ANASEMA KUWA YEYE NI MMOJA KATI YA MIAMBA YA BUCHOSA NA AMEKUWA KIPENZ NA KIVUTIO KIKUBWA CHA WATU



DANCER WA NYAKABAYA HATIRI ZAIDI




HUYU NDIYE NYAKABAYA MWENYEWE AU CHABHANYA  (MIAMBA YA BUCHOSA)



Friday, January 9, 2015

DIAMOND: SIAMINI KUPEWA NAFASI!

 
Staa Afrika Mashariki, Nasibu Abdul ‘Diamond’ akipozi.
 STAA Afrika Mashariki, Nasibu Abdul ‘Diamond’, amefunguka kwamba haamini kama kweli amepata nafasi ya kutumbuiza kwenye sherehe za utoaji tuzo za wanamichezo bora zilizoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF) ambazo zimefanyika usiku wa kuamkia leo jijini, Lagos, Nigeria.
 Akizungumza na Showbiz, Diamond alisema amefurahi kupata nafasi ya pekee ambayo mara nyingi hutolewa kwa wasanii wakubwa Marekani na kuamini kwamba muziki wa Tanzania unathaminika kila kona.
 “Nimefurahi maana hii inaonyesha jinsi gani muziki wetu umekuwa hadi kufikia Afrika kuwa moja ya kionjo hasa kwenye tamasha kubwa kama hilo, kiukweli sikuwahi kufikiria hapo mwanzo,” alisema Diamond. 
 Mwaka jana, Diamond aliweka rekodi ya aina yake kwa kupokea tuzo nyingi hapa nchini, ikiwemo tuzo ya Ijumaa Sexiest Bachelor ambayo ilikuwa imedhaminiwa na Kampuni ya Kijumoz Intertraders CO. LTD, ambao pia walitoa ofa ya mshindi huyo mara tu atakaporejea nchini akitokea Nigeria kwenda kwenye maduka yao yaliyopo Kinondoni kwa Manyanya, Kinondoni Mkwajuni na Sinza kufanya shopping ya mavazi kuanzia juu hadi chini.

Friday, January 2, 2015

NAIBU WAZIRI WA WIZARA YA UCHUKUZI DK. CHARLES TIZEBA ATEMBELEA CHUO CHA BAHARI DAR ES SALAAM (DMI) MWANZONI MWA WIKI


DSC_0703
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba akisaini kitabu cha wageni katika ofisi ya Mkuu wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), mara baaada ya kuwasili chuoni hapo kuangalia shughuli mbalimbali zinazofanywa na chuo hicho na kuongea na wafanyakazi wa Chuo hicho, mwanzoni mwa wiki. Kulia kwake anaemtazama ni Kaimu Mkuu wa Chuo hicho, Kapteni Yasin Songoro.
DSC_0712
Mkufunzi wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), akimpa maelezo ya namna ambavyo wahandisi wanaofanya kazi ndani ya chumba cha injini ndani ya Meli wanavyoendesha mitambo hiyo kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba, wakati alipotembea chuoni hapo mwanzoni mwa wiki kuongea na wafanyakazi wa chuo hicho.
DSC_0719
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba, akimsikilza Kapteni Jumanne Karume, alipokuwa akimpa maelezo ya namna nahodha anavyoendesha Meli, wakati alipotembelea Chuo Cha Bahari Dar es Salaam(DMI), mwanzoni mwa wiki. Kushoto kwa Dk Tizeba ni Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Kapteni Yasin Songoro.
DSC_0721
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba (aliyeweka mikono mfukoni), akimsikiliza Kapteni Peter Mkunja wakati akimpa maelezo ya namna vyombo vya kujiokoa vinavyotumika endapo meli itazama ama kupata hitilafu yoyote, wakati Naibu Waziri huyo alipotembelea Chuo hicho Mwanzoni mwa wiki.
DSC_0722
Kaimu Mkuu wa Chuo Cha Bahari Dar es Salaam (DMI), Kapteni Yasin Songoro, akitoa maelezo ya namna ambavyo mashine inayotengeneza vipuri vinayoharibika ndani ya meli inavyofanya kazi kwa Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba, alipotembelea Chuoni hapo Mwanzoni mwa wiki hii.
DSC_0724
Sehemu ya Menejimenti na wafanyakazi wa Chuo cha Bahari Dar es Salaam (DMI), wakimsikiliza Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba (Hayupo Pichani), wakati alipoongea nao mwanzoni mwa wiki.
(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi)

Jokate: Diamond Hana Akili Timamu


Jokate: Diamond Hana Akili Timamu
Mrembo na mwanamitindo ambae pia ni mwigizaji wa filamu na ujasiriamali, Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ amemrushia maneno makali aliyewahi kuwa mpenzi wake, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ kuwa hana akili timamu kufuatia maneno aliyotoa kuwa enzi za uhusiano wao, eti mwanadada huyo alikuwa akichenga kumzalia mtoto.
Hivi karibuni akizungumza na Global TV online, Diamond alifunguka: “Jokate na Wema (Sepetu) nilitamani sana wanizalie lakini walikuwa wakichengachenga, mambo mengine ujue si ya kuzungumza lakini inauma.”
Kufuatia tuhuma hizo nzito huku kukiwa na madai pia, kwamba Jokate aliwahi kupigwa mimba ‘akaipanchi’, mwanadada huyo alipotafutwa na mwandishi wetu kujibu ‘shitaka’ linalomkabili alianza kwa kumshangaa Diamond.
Jokate alisema anamshangaa Diamond kuyazungumza maneno hayo hadharani na inaonesha asivyokuwa na akili timamu au ambayo haijakomaa.
 “Diamond atuache, kila siku anatuzungumzia, hana akili timamu.
“Inadhihirisha kweli hana akili kwa kuwa mtu mwenye akili zake timamu hawezi kwenda kwenye chombo cha habari na kueleza hayo aliyoyasema,” alisema Jokate akionesha kukasirishwa na maneno ya Diamond.