Wednesday, December 17, 2014

AISHA MADINDA AFARIKI DUNIA KIFO CHA UTATA, MWILI WAKUTWA HOSPITALI YA MWANANYAMALA


Aliyekuwa mnenguaji Mahiri wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta' Aisha Madinda, amefariki dunia katika mazingira ya kutatanisha na mwili wske umegundulika ukiwa umehifadhiwa Hospitali ya Mwananyamala mchana huu.

Akizungumza na kwa njia ya simu, Mkurugenzi wa bendi ya Twanga Pepeta, Asha Baraka, alisema kuwa alipewa taarifa na Daktari mmoja kuwa wameona kama mwili wa Aisha Madinda hospitalini hapo, ndipo akatuma watu kwenda kuangalia akiwemo Luiza Mbutu ili kuhakikisha kama kweli ni yeye ndipo walipogundua ni yeye.

“ Mimi nipo njiani natoka Kigoma kuja Dar es Salaam, ni habari ya kusikitisha sana maana Aisha amefariki katika mazingira ya kutatanisha sana, jana alikuwa mzima na anachati na watu kwenye simu leo napigiwa simu mwili wake umekutwa umehifadhiwa hospitali ya Mwananyamala, hata sielewi nini kimetokea”. Alisema Asha Baraka

Naye Meneja wa bendi hiyo, Hassan Rehani, akizungumza kwa njia ya simu na mtandao huu, alisema kuwa, ''Aisha Madinda amefariki dunia, kifo cha utata na mwili wake umekutwa hospitali ya mwananyamala, haijulikani aliyeupeleka,

Bado Uongozi wa Twanga tupo eneo la tukio hapa hospitani tukisubiri majibu kuhusu utata huo, je ni nani aliyepeleka mwili huo hospitalini hapa kwani inaonyesha alifilishwa hapa akiwa tayari amekwishafariki''.alisema Hassan
Mungu ailaze roho ya Marehemu Aisha Madinda mahali pema peponi , Amina

No comments :

Post a Comment